FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Wednesday 16 July 2014

KUMBE WASANII WA BONGO NI WASHIRIKINA WA KUTUPWA, KAZI KULOGANA TU??


 
Staa  wa  kike  anayefanya  vizuri  katika  tasnia  ya  muziki  na  filamu  nchini, Baby  Joseph  ‘Baby Madaha’  amewatolea  uvivu  wasanii  wenzake  kwa  kuifumua  tasnia  hiyo  kuwa  asilimia  kubwa  ya  wasanii  ni  washirikina  na  wanalogana….

Msanii huyo  amewashutumu  baadhi  ya  wasanii  Bongo  kuwa  hawawezi  kufanya  jambo  lolote  muhimu  bila  kufanya  ushirikina  na  wengine  hawapendi   kuona  wenzao  wakitoka  kimaisha…..

Madaha  amefikia  hatua  ya  kufumua  ushu  hiyo  kwa  madai  kuwa  hata  kufilisika  kwake  ghafla  kumetokea  baada  ya  aliyekuwa  mpenzi  wake  raia   wa  Kenya  Joe  Kairuki  kupunguza  nguvu  ya  kumsaidia  kisanii  na  kwamba  ilitokana  na  rafiki  zake  kumpiga  juju….

Soma na hii=>SHILOLE AWASHANGAA WANAO KAA NA KUCHONGA KUWA MPENZI WAKE NUHU NI SERENGETI BOY

“Wasanii  wenzangu  wameniloga.Walikuwa  wanaona  donge  sana  Joe  alipokuwa  akinisaidia.Kiukweli  wameniporomosha  kabisa.Nilienda  kwa  mtaalamu  akanithibitishia  hili.Hata  hivyo  nimepata  mfadhili  mwingine.Siwezi  kumtaja  wasije  wakanipiga  kipapai  tena,”  alifunguka  staa  huyo  wa  wimbo  wa  Summer Tyme.

Alisema  ushirikina  umeifanya  tasnia  ya  sanaa  kudumaa  kwa  kiasi  kikubwa  na  kwamba  imani  hiyo  imesababishwa  na  wsanii  wasio  na  elimu….

SOMA NA HII=>HII NI KUHUSU BIFU KUBWA KATI YA PENNY NA BABY WEMA SEPETU!! SOMA HAPA

“Wasanii  wachawi  wapo  wengi  tu.Yaani  unamuona  msichana  mzuri  au  mvulana  mtanashati  msanii  kumbe  anakesha  kwa  waganga.

“Wengi  wanasafiri  sana  kwenda  mikoani  kuloga  wenzao.Sanaa  imejaa  uchuro  mtupu. Kama  si  kuelemewa  na  ushirikina  basi  tungekuwa  mbali  sana.

SOMA NA HII=>NU-DE PHOTO ALERT: TAZAMA PICHA HIZI ALAFU UTOE YA MOYONI ETI NI MSAANII MKUBWA HUKO NIGER

“Ushirikina  umesababisha  pia  fitina, majungu  na  visilani  miongoni  mwa  wasanii. Hatupendani  kwa  sabab  ya  mioyo  ya  kichawi,” Alisema  Baby  Madaha

No comments:

Adbox