FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Friday 1 August 2014

UNAAMBIWA MUME WA JACK CHUZ ANUSURIKA KUFA APATA AJALI MBAYA SANA


MUME wa msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuzi’, Gadner Dibibi amesherehekea Sikukuu ya Idd vibaya baada ya kupata ajali wakati akienda msikitini.



Mume wa msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuzi’, Gadner Dibibi akionyesha majeraha baada ya ajali hiyo.
Chanzo cha habari kilitiririka kuwa, Gadner alipata ajali hiyo maeneo ya Mlimani City alipokuwa akishuka kwenye Bajaj ambapo Bodaboda ilimpitia na kumgonga.
Msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuzi’, Gadner Dibibi wakati wa harusi yao.
“Ameumia sana, alikuwa akienda kuswali swala ya Idd lakini kwa bahati mbaya ajali hiyo ikatokea,” alisema mtoa habari huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.Gadner alipoatikana alikri kupata ajali hiyo na kueleza kuwa, kwa sasa anaendelea kuuguza majeraha.

No comments:

Adbox