Ilidaiwa kuwa, warembo hao waliambiwa mapema kuwa ifikapo alfajiri wasionekane kwenye eneo la baa hiyo lakini wao waliendelea kupombeka mpaka jua linachomoza ndipo mabaunsa walipowaondolea uvivu kwa kuwapa kipigo.
Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, hasa wanaume walisikika wakipongeza kitendo cha warembo hao kuchezea kichapo wakisema wamezoea kukesha eneo hilo mpaka kunakucha.
Mashuhuda hao walikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa wanahisi warembo hao wanajihusisha na biashara ya ‘udada poa’.
Kilio kikubwa cha mabaunsa hao kilikuwa ni kutaka kusimamia heshima ya baa hiyo kwa vile wateja wanaofika hapo ni wenye heshima zao.
“Msije tena hapa, sisi hatuwataki muda wa asubuhi wala mchana, tulishasema sana lakini hamsikii, mnataka kutukimbizia wateja siyo?” alisema mmoja wa mabaunsa hao.
No comments:
Post a Comment