FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Wednesday 16 July 2014

MPYA! RICH MAVOKO AUKANA WIMBO "TURURU" ULIOTOKA JANA KWA JINA LAKE



Rich Mavoko amekana kuachia wimbo mpya unaoitwa ‘Tururu’ wimbo ambao ulisambaa sana jana kwenye mitandao ya kijamii na websites na kupata namba nzuri ya watu walioupakuwa.
Akiongea na tovuti ya Times Fm, Rich Mavoko amesema binafsi ameshangaa baaad aya kusikia kuwa ametoa wimbo mpya na kwamba wimbo huo sio wimbo mpya, ni wimbo aliourekodi miaka mitano iliyopita na hana mpango wa kuutoa.

“Sio ngoma mpya, cha kwanza nachoweza kusema. Si ngoma ambayo nimeitoa mimi. Yaani sijui nani ameileta, blog gani inafanya hivyo vitu. Kwa sababu ni ngoma ambayo nimeirekodi miaka mitano nyuma. Can you imagine ni ngoma ambayo nimeifanya hata kabla sijafanya Silali.” Rich Mavoko ameiambia tovuti ya Times Fm. Ameeeleza kuwa hii sio mara ya kwanza watu kuvujisha nyimbo zake na yeye anaonekana kama anavujisha ngoma.

Mavoko amezungumzia pia mazingira ya kuvuja kwa wimbo huo ambao ameurekodi katika studio za Sharobaro chini ya producer Bob Junior. “Sipendi kumlaumu producer wa hiyo kitu kwa sababu pia hata yeye anaweza kusema mimi nilikupa hiyo nyimbo. Kitu ambacho mimi nakumbuka mara ya mwisho hii nyimbo inakuja kuvuja..hii nyimbo, nilishawahi kuwa na meneja hapo nyuma..sipendi kumuongelea. Nyimbo zangu nyingi baada ya kuachana na mameneja zinavuja yaani. Sipendi kumuongelea vibaya yeye lakini hii kitu inaniudhi.” Ameeleza.

Amesema kitu kinachomuumiza zaidi ni tofauti ya uwezo wake wa kuimba miaka mitano iliyopita unaosikika kwenye wimbo huo ambao ni tofauti kabisa na uwezo wake wa sasa.
Msikilize hapa kwa urefu:

No comments:

Adbox