FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Saturday 19 July 2014

IRINE UWOYA AZUNGUMZIA JUU YA TUHUMA ZA KUCHEPUKA NA MUME WA MTU




Nyota wa sinema za Kibongo, Irene Uwoya amefunguka juu ya tuhuma za kufanya fujo nyumbani kwa mume wa mtu zilizoripotiwa na mitandao mbalimbali ya habari nchini hivi karibuni.

Akizungumza exclusively nasi, Irene amesema kuwa haelewi hizo tuhuma zimetoka wapi na wala hajui aanzie wapi kuzijibu maana siyo yote yaliyoripotiwa ni kweli.

Tuhuma hizo zilidai kuwa, mwanadada huyo mrembo alienda kuleta timbwili nyumbani kwa mume wa mtu huyo baada ya kusikia kuwa jamaa huyoa ameamua kuoa na kumoiga chini Irene aliyekuwa akitoka naye kipindi cha nyuma.

TOP 3 LOL!! UNAAMBIWA MCHUNGAJI MTIKILA AMFUNGULIA KESI ASKOFU MOKIWA KWA KUMSHIKA MAKALIO HADHARANI.!

“Uwoya alitegemea angeolewa yeye, sasa kusikia jamaa kaoa mwanamke mwingine tena kwa siri, ilimfanya aishiwe nguvu,”Habari hizo ziliriripoti.

Habari zinazidi kudai kwamba, alichoamini Uwoya ni kwamba kitendo cha mwanaume huyo kuoa kingemfanya yeye aendelee kuwa ‘nyumba ndogo’ jambo ambalo hakupenda kulisikia hata kidogo.

Akifafanua tukio hilo Zaidi uwoya alisema.
“Ilitokea, lakini nilishaachana naye. Unajua ishu si kwamba angenioa mimi, ila kitendo alichokifanya hakikuwa cha uungwana,” alisema Uwoya.

No comments:

Adbox