Kocha wa Brazil Luiz Felipe
Scolari ameagiza mwanasaikolojia kujiunga na kambi ya mazoezi ya timu
hiyo kufuatia ushindi mgumu dhidi ya mahasimu wao wakuu Chile.
Wenyeji hao wa kombe la dunia walihitaji muda wa
zaida na bahati kuilaza Chile mabao 3-2 jambo lililowaacha wengi wa
wachezaji wao akiwemo Neymar wakitoa machozi baada ya mechi hiyo katika
uwanja wa Estadio Mineirao.Brazil atachuana na Colombia katika robo fainali siku ya ijumaa.
Matumaini ya wenyeji ni kuwa Neymar ataiongoza timu hiyo kunyakua kombe la dunia .
Mshambulizi huyo wa Barcelona mwenye umri wa miaka 22 tayari ameifungia timu yake mabao manne.
No comments:
Post a Comment