Arsenal, Liverpool hapatoshi ligi kuu

Wachezaji wa Arsenal wakishangilia goli katika mojawapo ya mechi walizocheza ligi kuu ya England
Ligi kuu ya England inaendelea
kwa vinara wa ligi hiyo Arsenal kupambana na Liverpool inayoshika nafasi
ya nne kati msimamo wa ligi hiyo.
Liverpool inawakaribisha Arsenal katika uwanja
wake wa Anfield, ikisaka pointi tatu muhimu ili iweze kujiimarisha zaidi
katika kinyang'anyiro cha ligi hiyo, huku Arsenal nayo ikizitaka pointi
hizo ili kuzidi kuweka pengo na wapinzani wake wakuu Manchester City na
Chelsea zinazowania taji la ubingwa wa ligi hiyo.
Wachezaji wa Liverpool wakishangilia goli katika mojawapo ya mechi zao
Olivier Giroud, Santi Carzola, Mesut Ozil na Oxlade-Chamberlain wakihofiwa kulitia msukosuko lango la Liverpool.
Kwa ufupi ni mchezo muhimu kwa kila timu katika kuwania taji la ubingwa wa ligi kuu ya England na pia kujiweka katika mazingira mazuri ya kufuzu kucheza kombe la mabingwa barani Ulaya.
No comments:
Post a Comment