FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Monday 23 November 2015

The Game kaamua kuisogeza list yake ya rappers 10 wakali zaidi duniani, Eminem na Ice Cube watajwa!


Orodha ya The 10 Greatest Rappers of All Time ya Billboard inaendelea kuweka headlines tofauti kwenye mitandao ya kijamii… siku chache tu zilizopita tulishuhudiaSnoop Dogg akisema kutokuwepo kwa 2 Pac kwenye orodha hiyo ni kitendo ambacho hakikuzingatia masharti na ubora wa muziki wa Hip Hop, Marekani.
Haikuishia hapo, kwa upande wa Bongo Flevani napo tulishuhudia msanii wa Bongo Fleva, Nikk wa Pili akiitoa list yake ya rappers 10 wakali wa Tanzania… na leo msanii wa HipHop kutoka Marekani, The Game ameona na yeye aisogeze list yake ya rappers 10 wakali zaidi…. watu walioguswa?!
bill4
Kupitia page yake ya Instagram, The Game alipost list yake na caption ya maneno iliyosema…
>>> “Billboard wanavuta bangi sio bure!!! Inabidi niwarekebishe maana huu ni uzembe na kosa kubwa kwa HipHop… na naomba mnielewe MSIRUDIE TENA KUFANYA KOSA LA NAMNA HII KWENYE ARDHI YA MUNGU, LA KUTENGENEZA LIST YA HIP HOP BILA KUMUWEKA 2PAC @SnoopDogg au @Icecube #F*BillboardList“<<< @losangelesconfidential.
bill
Baada ya kuandika caption hiyo, The Game akaiweka hewani list yake ya rappers 10 wakali zaidi duniani… na kuiita list hiyo ‘MY LIST’
10 Greatest Rappers Of All Time (Kwa mujibu wa The Game) ni….
1. 2pac & B.I.G
2. Nas
3. Rakim
4. Eminem
5. Jay-Z
6. Ice Cube
7. Snoop Dogg
8. Andre 3000
9. Jadakiss
10. Big L & F** YO OPINION !!!!!!!!!”
Je hapa vipi mtu wangu, unakubaliana na The Game? Au na yeye kuna watu muhimu kwenye game hajawagusia!
?

No comments:

Adbox