FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Wednesday 23 July 2014

WEMA SEPETU SASA AJUTA KUTUMIA MKOROGO... AELEZA KILICHOMTOKEA, INASIKITISHA SANA:


MISS Tanzania 2006/07 Wema Sepetu amesema ugonjwa wa ngozi ulioshambulia sehemu ya shavu lake la kushoto umeharibu urembo wake na kumfanya ashindwe kutoka.

Akizungumza kwa huzuni, Wema alisema hakutegemea kama tatizo hilo lingekuwa kubwa, kwani lilianza kama kipele kidogo ambacho baadaye sehemu kubwa ilivimba na kuharibu mwonekano wake.
 
“Ulianza muwasho, kikawa kipele kisha kikageuka kama kishilingi.
 
Nilipokwenda hospitali nilipewa dawa ya crime ya kupaka, mimi nikachua eneo lililoathirika, kumbe ndiyo nikawa nasababisha matatizo, kukavimba zaidi kama unavyoona,” alisema Wema ambaye alikataa kupigwa picha.

No comments:

Adbox