FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Wednesday 30 July 2014

MASKINI DUDE, HALI TETE SASA BAADA YA KUHUSISHWA NA NJAMA ZA UJAMBAZI NA USHAHIDI HUU HAPA


GARI la muigizaji maarufu wa filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ limekamatwa na Polisi jijini Dar es Salaam likihusishwa na tukio la ujambazi linalodaiwa kutokea Kijitonyama Mpakani usiku wa saa 5.15 Julai 21 mwaka huu.


Gari la dude muda mfupi baada ya kukamatwa, Dude alitokea Polisi.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, gari hilo aina ya Vitz lenye namba za usajili T 360 BAJ, lilikutwa likiwa na vijana wawili ndani yake, waliotajwa kwa majina ya Seif Jafari na Longina Ramadhani, waliotaka kupora Bajaj yenye namba za usajili T 296 CSC iliyokuwa ikiendeshwa na Seleman Khalfani.

Inadawa kuwa muda mfupi baada ya kukamatwa, Dude alitokea Polisi na kulitambua gari lake, lakini maelezo yake hayakuwatosheleza Polisi hivyo kumshikilia katika kituo kidogo cha Polisi Mabatini hadi kesho yake alipodhaminiwa.                                                              Muonekano wa gari hilo kwa nyuma.
Waandishi wetu walifanya jitihada za kumtafuta Dude ili azungumzie taarifa hizo, lakini aliwataka kufuatilia jambo hilo katika kituo cha Polisi, akisema suala hilo lipo mikononi mwao.

Kulwa Kikumba ‘Dude’
Shauri linalomkabili msanii huyo limefunguliwa kwa Jalada namba .KJL/RB/6399/14 UNYANG’ANYI

No comments:

Adbox