Mama mzazi wa star anayeipeperusha vizuri bendera ya Tanzania kimataifa
kwa sasa kupitia muziki, Nasib Abdul a.k.a Diamond Platnumz jana (July
11) alipata nafasi ya kuzungumza na paparazi, mambo mbalimbali
yanayomhusu mwanaye.
Haya ni baadhi ya maswali ambayo aliulizwa na paparazi, pamoja na majibu
aliyoyatoa:Kuhusu tuhuma za Diamond kujihusisha na ushirikina katika
muziki wake:
“Hiyo si kweli na wala hana ushirikina, si unajua tena mtu ukiwa juu
kila mtu atakusingizia anachowaza yeye ili apate sifa
ajulikane…Havijatokea watu uzushi tu wanapenda sasa ushirikina wa nini ,
kama mtu upo juu upo juu kama upo chini upo chini, nay eye sasa hivi ni
nafasi yake kama sio nafasai yake atashuka walikuwepo wangapi,
alikuwepo Mr Nice alikuwepo juu, lakini zamu yake imefika imeshuka
imekuja zamu ya Nasib wacha awe juu itakapofika yake kushuka atashuka”.
Na hii tabia ya mara (msichana) huyu mara huyu wewe ukiwa kama mama kwako huo unaipokea vipi?
“ Siipokei vizuri laikini sasa nitafanya nini nay eye star, wengine
wanajitongozesha bila kutongozwa..mi mwenyewe hapa kutwa napigiwa simu
mpaka nazima, wananipigia simu wanafikiria Nasib wanajitongozesha mpaka
nawatumia meseji mbona mnajitongozesha, hii sio namba ya Nasib hii namba
katoa ya biashara ya Tshirt 0716186318 sio namba ya Diamond, namba yake
mama yake.sitaki usumbufu..wananitumia mapicha ya uchi , mapicha ya
nini sasa ni ustarabu gani huo.Credit:TheChoice
No comments:
Post a Comment