FACEBOOK

LightBlog

Breaking

LightBlog

Wednesday, 5 February 2014

MSANII MATONYA AFANYA UTAPELI WA KUTISHA LUDEWA NJOMBE ,AKIMBILIA POLISI KUJINUSURU NA KICHAPO


MSANII  wa  muziki wa kizazi kipya ambae ametamba na nyimbo  mbali mbali ikiwemo Anita na Violet na nyingine ,msanii Matonya  ameponea katika tundu la sindao kupokea kichapo cha mbwa  mwizi  kutoka kwa  wapenzi wa muziki huo mjini Ludewa mkoa wa Njombe  baada ya  kuwatapeli  fedha zao za kingilio bila ya kuonyesha  show kama mashabiki walivyotegemea.

Matonya  ambae  alipaswa kufanya  show hiyo katika ukumbi wa Resort  mjini Ludewa  jana alikwama kufanya hivyo na badala  yake alilazimika  kukimbia eneo la ukumbi na kwenda  kujisalimisha  kituo cha  polisi kufuatia jazba za wapenzi  wake ambao  walitaka arudishe  fedha za kiingilio ambazo  walitoa kiasi  cha Tsh 4000 kwa kila kichwa .

Msanii  huyo ambae  alifika nje ya  ukumbi  huo toka mida ya saa 2 usiku akiwa katika gari ndogo aina ya Taxi nyeusi  pamoja na  promota   wake  wakiendelea  kuchangisha  fedha za madafu kutoka kwa  wakazi wa Ludewa kwa maana ya  kuwatoza kingilio  huku Matonya akiwa  mbele ya gari hiyo kwenye usukani akiendelea  kuvuta  sigara na kula kinywaji  huku  promota  wake akiendelea  kuwachojoa    pesa za kiingilio  mashabiki  waliokuwa  wakitaka kuona show  hiyo.

Kama haitoshi mida ya saa 6  usiku  hali ya  wasiwasi  ilianza  kujitokeza ukumbini  humo baada ya mashabiki  kutoka nje ya  ukumbi  wakitaka  msanii  huyo kupanda jukwaani kutokana na muda kuendelea  kuyoyoma bila  ya  Matonya  kuingia  ukumbini .

Hali  hiyo  ilipelekea  vurugu za hapa na pale  kutokea  kwa mashabiki hao na uongozi wa ukumbi  huo  na baada ya muda  polisi  kufanikiwa kuzima vurugu hizo na mashabiki  kulazimika kuingia ndani ya ukumbi kwa kutulizwa na nyimbo za wasanii  wengine kama bolingo ,taarabu na nyimbo za Diamond   .

Ili  kuwa ni majira ya saa 7 .15  usiku ndipo matonya  alipojitokeza ndani ya  ukumbi huku meneja wa ukumbi  huo akiwasha taa na kuwataka  mashabiki kujiandaa  kupata  burudani  ila haikuwa hivyo kwani Matonya alipanda  jukwaani  bila ya  kisemeo (mic) na kuongea kwa sauti ya juu kuwa Mic  haipo anaomba  ipigwe nyimbo  yake  ili  acheze na  wadau  wake hali  iliyopingwa na kuanza  mzozo ukumbini hapo.

Kutokana na mzozo huo ambao  ulipelekea  mashabiki kumtaka Matonya  kuimba  chini ya ulinzi bila ya kuwekwa  CD katika radio ndipo Matonya  alipotafuta  upenyo  na  kukimbia ndani ya Ukumbi  huo kutokana na kushindwa  kutimiza matakwa  ya wadau wake  waliotaka  kuimba live  bila  CD .

Kitendo cha Matonya  kutoka nje ya  ukumbi kiliamsha  haliya  vurugu  ukumbini huku  mashabiki hao  zaidi ya 20  wakitaka  kurudishiwa [pesa  zao kwa madai kuwa  zinatosha kwenda  kulipa  vibarua  wa kupalilia mahindi shamba .

Madai  hayo yalimfanya Matonya  kuingia katika Taxi  yake na  wapambe wake na kukimbilia kituo cha  polisi huku mashabiki hao  wakilifukuza gari hilo kwa kutaka kumwadabisha Matonya kwa utapeli .


Pona ya Matonya  ilikuwa ni kukimbia eneo hilo huku  polisi  wakilazimika kufika  eneo hilo kuwatawanya  mashabiki hao ambao  baadhi  walitangulia katika nyumba ya kulala  wageni ya Malaika  ambayo alifikia ili kumfanyia vurugu  bila mafanikio baada ya msanii  huyo kulazimika kuukumbia mji wa Ludewa usiku kwa usiku na kurejea Njombe .

Hata  hivyo mbali ya kuwatapeli  mashabiki hao  bado msanii  huyo  anadaiwa  kumliza mwenye muziki ambae ni afisa wa  serikali  wilaya ya Ludewa baada ya  kumtumia kianzio  cha Tsh 60,000 kati ya 150,000 za  kukodisha  vyombo vya muziki na kisha  fedha  hiyo ambayo aliituma kwa njia ya M- Pesa  kuirudisha  tena kwake .


Afisa huyo wa serikali amedai kuwa tayari amekwenda  polisi kutoa taarifa  ili kumsaka msanii  huyo popote alipo na kumfikisha mbele ya  vyombo vya  sheria .

Jeshi la  polisi  wilaya ya Ludewa limethibitisha  kutokea kwa vurugu  hizo na kuwa  bila ya polisi kufika mapema eneo hilo msanii  huyo angefanyiwa kitu  kibaya  zaidi na kuwa hadi sasa  wanamsaka Matonya  ili kufikia makubaliano na  wadau  wanaodai kutapeliwa fedha  zao  za kiingilio

No comments:

Adbox